HISTORIA YETU
UTANGULIZI
TANROADS SACCOS LIMITED ni Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Wafanyakazi wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS), waliokuwa watumishi wa Wakala ya Barabara (TANROADS) na Watumishi waajiriwa wa TANROADS SACCOS LIMITED.
USAJILI
Chama kiliandikishwa kwa mara ya kwanza Julai 27, 2006 na kupewa namba ya Usajili DSR 896. Mwaka 2021 Chama kilisajiliwa kwa mujibu wa Sheria Na. 10 ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 na kanuni zake za mwaka 2019 na kupewa Leseni ya Mtoa Huduma Ndogo za Fedha namba MSP3-TCDC/2021/0418.
Hata hivyo mnamo Mei 03, 2023 Chama kilisajiliwa upya na TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA TANZANIA (TCDC) na kupewa namba mpya ya usajili PRI-DAR-DAR-CC-2023-5373
